

Hii ni video ya pili ya mtu mzima Moracka, video hii picha zake ziko tofauti tofauti, shoti hizi za mwanzo zinamuonyesha Moracka akiwa ndani ya lift halafu anaingia mrembo ndani ya lift hiyo na baada ya lift kufunga ndio utapata matukio mengine huku lift ikishuka chini.

Hapa inawaonyesha wakiwa ndani ya lift na Moracka akionyesha kumtamani kinoma huyu binti kumbe binti ana jamaa wake anamsubiri kwa chini.

Huyu ndio jamaa mwenyewe anayemsubiri yule binti ambaye yuko kwenye lift ashuke chini.

Mwanadada ameshashuka na jamaa wake inabidi asepe nae, mwisho wa video ndio utaona haya na utanielewa nachomaanisha.

Raya akiwa na dj choka wakati walipokuja kushuhudia video ya Moracka

Rosemina, Moracka na Dau Racka

dj choka na mwanadafada Suzy, Pole Suzy kwa kuibiwa simu wakati unarudi home
Rechal, Nuru, Nas 3 na Rose

Tugeza tunawakilisha.

huyu ndiye beauty wa wiki ile iliyopita anaitwa Nancy Summary, alipata kura 102 sawa na asilimia 72 huku akimwacha mwenzake ambaye alikuwa Nakaaya kwa kupata kura 39 sawa na asilimia 27.
Asante wadau wangu.

Msanii Moracka leo mchana atafanya video yake ya wimbo wake mpya unaoitwa
SHE GOT IT ambao amemshirikia mwanadafada
DIVA. Moracka ameniambia video hiyo inafanywa na kampuni ya Kallage's Picture.

Maandalizi ya video huwa ni hivi, nikirudi nitakuja picha za video hii ikiwa inatengenezwa wadau.
Kitaani volume 1, ni mixtape iliyosheheni wasani wakali kama Fid Q, Jay Moe, Chidi Beenz, Witness, Solo Thang na wengine wengi inapatikana kupitia +255 714 884342.
CD inauzwa sh 5,000/=

Samaki ana mengi yakusema lakini mdomoni ana MAJI.

Anaitwa Rashid aka Chidi Beenz, nimsanii wa bongo fleva na mwaka jana ndio msanii aliyefanya kollabo nyingi sana na wasanii wa hapa kwetu na nje ya Tanzania.
Kulikuwa na shindano la kumtafuta msanii yupi atakuwa hot kwa mwaka jana na Chidi alikuwa anashindana na wasanii wenzake ambao ni FID Q, MWANA FA, PROF JAY, AY, JAY MOE, LORD EYES, MANGWEAR na JOH MAKINI.
Na matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:-
1. Chidi Beenz -
1572. Fid Q -
1333. Joh Makini -
1324. Mangwear -
1005. AY -
736. Mwana FA -
557. Prof Jay -
458. Jay Moe -
439. Lord Eyes -
35Haya ndio maneno ya Chidi Beenz baada yakumwambia umeshinda
"Duh nashukuru tu na nawapenda sana tuko pamoja na nakuja na kitu kinaitwa La Familia NWO. Hata wafanyaje itashindikana kunifikia, Chidi aka Big Boss aka King Kong aka CHUMAAH."Shukrani kwa wote walivote...nyie ndio mnaousimamisha mziki huu wa bongo fleva
Mungu ubariki mziki wetu wa Bongo Fleva.

Leo nilitembelea mahali fulani na ma homie Moracka, na menu letu lilikuwa kama hivi,
hapa ni kitu cha Nyama

Bwana wee hii hapa mtanisaidia kwa kweri daah

Pronsi kidogo si mbaya

Huyu samaki sasa usimpimie kabisa...hapa alikuwa amechambuliwa mifupa yote ndio kawekwa hivi bwana

Mtoto Moracka alichemsha, alikuwa anaanzisha ligi na mimi kwa kula.