Ni muda mrefu sana umepita tangu tujumuike pamoja pale Soma Mkahawani,sasa ni wasaha mwingine tena wa kujumuika pamoja na kusherehekea kwa pamoja kama ilivyofanyika kipindi kile.
Swali ni je mtapendelea tujumuike kwa pamoja lini,na wapi,na michango iwe ni kiasi gani kwa kila mwanakijiji????
na nyie mbona mnatunyanyasa hamna kazi ila kukutana itabidi mie na mama malaika hakupikwi wala hakulaliki mpaka mamr watukatie tiket na sie tuhudhurie au mama malaika unasemaje
Permalink Reply by Dada on Septemba 27, 2009 at 4:29pm
mmh, Jr. Umekuwa Padri au IMAM? Unaomba kusalisha au KUWASILISHA? Kuhus kukutana si jambo baya ila cha kufanya kwanza tutafute venue then tujue budget ya kujumuika kwetu, then tupange cha kufanya.
NOMBA KUWASILISHA
Cha ajabu sehemy ya kukutana huwa ni Dar tu! Sawa hatukatai, kwasababu dar kuna wanakijiji wengi, Lakini je inakuwaje hata wale watu wa dar mahudhurio yao huwa hafifu? Kesho ntawasilisha hoja nyengine, acha niwahi bia yangu
Mbona mnakutana mala kwa mala na hatupati mlichoongea na mmekubaliana nini kati ya hayo mliongea,mangapi hayaja tekelezwa?nafurahi sana mnapokutana hakika ni
UMOJA NI´NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU,
mtujulishe mtakayo jadiliana kwa namana moja au nyengine tumeshindwa kuudhulia
Nafikiri kila kwenye wadau wakutane huko waliko na lengo ni kuadhimisha uwepo wa Fotobaraza kama watu wako mbeya wakutane sehemu fulani kama morogoro wakutane mahali fulani kama dar wakunatane sehemu itakayo pendekezwa na hata wa nje kama uk wakutane maahali fulani watakapokubaliana na usa na kila mahali ambapo wadau wako karibu au sehemu inayoweza kuwakutanisha,napenda kutoa hoja.Kama mdau wa uk ningependa wadau wa uk tupendekeze sehemu ya kukutana ili na sisi tuwaunge mkono wenzetu na kufahamiana zaidi.
Nikweli Young!! inabidi wanakijiji wakila sehemu wakutane kutokana na urahisi wao!!!......wacha nipange na Mabagala nasisi wa Zanzibar, tukutane na tutoe mualiko kwa wanakijiji wengine!!