FotoBaraza.Net

Ni mara kadhaa wanakijiji wa FB tumekuwa tukikutana, iwe ni rasmi au si rasmi, sehemu maalum au kwa kuitana wachache tu, lakini kikubwa ambacho kinaniumiza kichwa na kushindwa kupata majibu sahihi ni hiki:

"NI YAPI MALENGO YA KUKUTANA KWA WANAKIJIJI?"

Tulipokutana SOMA (mahudhurio yalikuwa mazuri sana) tulipanga mambo mengi ya msingi ya kuzungumzia ikiwa ni pamoja na mijadala inayoendelea kijijini lakini pia kubwa mojawapo ikiwa ni utekelezaji wa yale ambayo tunayaanzisha kijijini, mfano "FOTOBARAZA FOUNDATION" na forum ndogondogo zinazojumuika na kufanya kijiji kiwepo. Kiukweli hatujawahi kufanikiwa kutekeleza japo nusu ya hata jambo moja kati ya yale tunayoyakusudia katika mikutano yetu.

Kwa mara ya pili tulikubaliana kukutana Msasani Beach Club kwa ajili ya kujadiliana "live" yale ambayo tunajadiliana kijijini, kwa bahati mbaya mkutano huo haukufanikiwa kuwa na mahudhurio mazuri na mwishowe tukatawanyika bila kutekeleza azma ya mkutano huo.

Wiki iliyopita Tarehe 7/11 wanakijiji wamekutana kwa ajili ya malengo yaliyopangwa lakini mwisho wa siku taarifa tulizozipata ikiwa ni pamoja na picha zilizopandishwa kijijini ziliashiria ya kwamba hakukuwa na jambo lolote la zaidi ya kunywa, kufahamiana na kuongea kisha kutawanyika bila ya kufanya lolote ambalo lingekuwa na muelekeo wa muendelezo wa kijiji chetu katika kufanikisha yale tunayoyakusudia.

FOTOBARAZA ni "Social network" kama ambavyo mwanzilishi Babukadja (Apongezwe) alivyoitambulisha kwetu, nasi wanakijiji tumekuwa humu katika kuendeleza, kukuza na kudumisha "Social network" hii,.

Labda nirudi kwenye swali la msingi; "NI YAPI MALENGO YA KUKUTANA KWA WANAKIJIJI?"

Ntafarijika kuwekwa sawa katika hili; Pascal, Chaoga, Oswald, Cha, Jr, Clara, RT, Dunda, Mama Malaika, Jino Moja, Mathew, Jack, Lucie, Mtoto Mzuri, Babukadja, na wengineo wote ambao ni wanakijiji tafadhalini naombeni sana mfikirie kwa kina na kuweka michango yenu ili tuwe na tija na ufanisi katika kuhakikisha kijiji chetu kinakuwa na manufaa kwetu na jamii nzima kwa ujumla.

Ni Changamoto tu, tupo kijijini kunufaishana na si kubezana na kurudishana nyuma!

Shirikisha Twitter

Jibu Hoja Hii

Michango ya Mjadala Huu

Nashukuru kaka kwa kukumbuka majukumu yako, tusiwape nafasi hawa wakoseaji wa makusudi watuchafulie kijiji chetu kwa lugha mbovu, tuwarekebishe mpaka wajifunze! Tusichoke, natumai Cha nae anafatilia kwa karibu zoezi husika.

Jibu Hoja Hii

Ni kweli STiba, nafuatilia.

Jibu Hoja Hii

Ewaa, sasa bwana mdogo naona tunaanza kwenda sambamba, hayo ndio walau majibu ya swali langu la mjadala, na si lile chaka ulilokua umeingia, natumai taratibu kwa kufata maelekezo ya Cha na Magere utafika mahala utakaa meza moja nasi wanafalsafa wa kale! Nashukuru umeanza kuerevuka!

Jibu Hoja Hii

Kujadiliana na Party wapi na wapi. Mi nafikiri muanzisha mada usingegusia suala la kukutana Tarehe 7/11/2009. na hili ndo limeleta ubishi na kutokuelewana, labda na mimi niungane mkono na Pascal aka Mabagala.

Jibu Hoja Hii

Kaka Elly rejea vizuri kichwa cha habari cha mjadala kisha soma kwa utulivu maelezo yaliyosherehesha mjadala, ukimaliza pitia michango ya Magere na Cha, halafu umalizie na mchango wa mwisho wa Mabagala, natumai ukimaliza tutakuwa tumevaa kiatu kimoja. Ahsante kwa changamoto.

Jibu Hoja Hii

Safi sana Dr.Stiba kwa hii hoja ni ya ukweli na yenye kuleta maana.nimekuwa nikuwauliza au kupiga simu ili nijue wenzangu mnakuatana lini au mko kwenye kikao mnaongelea nini.yepi na yatatekelezwa vipi,kama tumeielewa hii hoja si kubomoa bali ni kujenga pindi siku nyengine tunapokutana tuwe na mrejesho wa yale tuliyoyaongelea lakini ngoja niishie hapa ili nijue kwa wenzangu waliokutana watajibu nini zaidi ili hoja iendelee
Ahsanteni sana

Jibu Hoja Hii

Nashukuru Dunda kwa mchango wako. Tutaendelea kupeana mawazo ili tuwe na kitu cha msingi kijijini kwetu.

Jibu Hoja Hii

Naunga mkono hoja hii na kuwa na malengo siku zote ni muhimu kuliko kutokuwa nayo,hata kama utekelezaji unachelewa lakini siku moja yatatimia.
Kuhusu Fotobaraza Foundation,kuna viongozi wanapaswa kutoa taarifa nini kinaendelea ili tuone wapi tumekwama na ikiwezekana unaweza kuwekwa mjadala live ili wadau wachangie na kuona nini cha kufanya kwa pamoja ,kwa siku itakayochaguliwa na baada ya maoni ya wengi watu wakakutana na viongozi kujadili na kufanikisha utekelezaji wake.
Naomba kuchangia hoja.

Jibu Hoja Hii

Young tumekusoma mkuu, maoni yako mwanana natumai yamewafikia wahusika japo wamejikausha kana kwamba mada hii hawaioni! Jr, Maingu, Babukadja na wengineo mbona hatuwasikii jamani?

Jibu Hoja Hii

Asante kwa kunikaribisha kaka,Naelezea kama ifuatavyo:
Mathumuni ya kukutana kwa wanakijiji, Inategemea na watu walivyopanga.
1.Tunaweza tukapanga kwamba tukutane kwaajili ya kujadiliana kuhusu foundation na mengine mengi
2.Tunaweza tukapanga kwamba leo tunasheherekea tu hakuna kujadili wala nn hivyo tunafurahia na kula mema ya nchi

Hivyo basi hiyo ya juzi ni kama walipanga kukutana na kuparty si unaona walivyotoka ki pati pati? hakuna kilicho haribika pale mana tutapanga tena siku ya kujadili na tutahudhuria tu. Asenti

Jibu Hoja Hii

Shukran twayyiba dada Lucie, nimekupata sawia, lakini nawe umekumbwa na upepo wa mfano wa mwisho wa mkutano wa tarehe 7/11. Hata hivyo umeeleweka uzuri. Lakini samahani neno "Madhumuni" asili yake ni "dhumuni" na si "thumuni" kama ulivyoandika wewe "Mathumuni!"

Jibu Hoja Hii

hahahaaa ok

Jibu Hoja Hii

RSS

Besdei za Kuzaliwa

© 2010   Created by Babukadja on Ning.   Create a Ning Network!

Beji  |  Report an Issue  |  Faragha  |  Terms of Service

Sign in to chat!
Free Web Counter
Hit Counter