Kuna habari imeripotiwa kuwa hadi sasa watu 12 ambao ni moja ya wapenzi wa mwanamuziki maarafu wa Pop duniani (Michael Jackson) aliyeaga dunia wiki iliyopita, nao wameamua kufupisha maisha yao kwa kujiua (commit suicide) sababu ya majonzi. Sizani Michael Jackson mwenyewe angependa kitu hiki kitokee kwa wapenzi wake.... Sijui wenzangu mnaonaje hoja hii...????
mama m nilitaka nikuulize kama ulikuwa bado hujakata tkt? kumbe nawewe unalo ok! ninini majaliwa ya hayo makaratasi mkononi ndio mtafanya kusamehe nakujumuisha kwenye rambirambi au nanyie mtadai kama desi na wanachama wao?
Araway..... Hilo karatasi nalitunza kama diamond wala sitaki refund. Tayari world leading collectors wameshaanza kuzitafuta hizo tickets kwenye internet, na wako tayari kuzinunua bei mara mbili tuliyolipia. Mwaka 2007 Kuna mtu London kauza ticket ya Elvis Presley kwa pound 7,000 (sawa na 14mil tsh) aliyonunua 1973.
Mwenzenu kamba ilikatika kabla ya kufikia lengo lenyewe!. maumivu niliyoyapata na kigugumizi cha kupumua kilichoniandama niliogopa kuchukua kamba ya pili na hivyo kusitisha zoezi zima la kumfuta the JACKO.
Pole sana Magere..... nafikiri roho mtakatifu alikushukia na kunena kwa lugha kabla ya kufikia lengo lenyewe ulilokusudia. Ila Cherry akija huko sijui kama kutakuwa na usalama. LOL............
Mama M bongo pia wanajiua ila wenzetu wametuzidi wanaweza wakateketeza familia nzima kwa stress.Nakumbuka vizuri niko Forodhani secondary,msichana wa Foro primary alijiua sababu mvulana wa secondary kamuacha.Mama yangu mkubwa akaniuliza kwani wanaume wamekwisha? Kwahiyo watu wanaposhindwa kua na alternative ndio uchukua uamuzi huo.
Hawa wenzetu wanawake zao hawana mbungi kabisa wanapoachwa na wala hutosikia kajiua... sijui sababu wanawake ni mapepe sana????
Kujiua hapa na barani ulaya kote wanaume ndio wanaongoza, ukute hao wote waliojiua kwa ajili ya Michael Jackson 10 ni wanaume au ukute hakuna mwanamke kabisa. Sijui wana akili gani au ndio malezi tokea utoto wanashindwa kustahimili? Ujue hata sie bongo tuna stress kuzidi wao..... ukizingatia extended family zetu huko Africa basi wajikuta kila siku stress haziishi lakini tunastahimili. Wao wazungu wakuta ni mume, mke na mtoto (watoto), lakini shida ndogo tu ya kifedha (finacial melt down) mtu alishajipiga risasi. Lakini wewe unayezungukwa na extended family unajipa moyo, iko siku mambo yatajipa. Wala hufikirii kujiua.
Pia angalia watoto wa shule wanavyoua watoto wenzao kwa bunduki nchi zilizoendelea, watoto wa kibongo waliokulia shida hata siku moja sijasikia kaenda kuwatungua roho watoto wenzie darasani.