Wewe ni mvulana mwenye umri wa miaka 30, Umelewa na upande mmoja tu yaani baba pekee, kila ukiuliza mama yako, baba hakupi jibu la maana, katika pilipilika zako za kutafuta maisha unahamia nji mwingine mbali na baba yako, unabahatika kupata kazi na unaamua kuoa, unaoa mke amekuzidi umri sana tu na mnabahatika kupata mtoto wa kiume, siku moja unaamua kurudi kwa baba ili umtambulishe Mkeo na mtoto. kufika kijijini baba mara baada ya kukuona badala afurahi anaangusha kilio, kuuliza kulikoni Baba anajibu ULIMUOA NI MAMA YAKO MZAZI. Sasa hapo nani wa kulaumiwa? BABA KWA KUKOSA KUONYESHA MAMA MZAZI WA MWANAE au MTOTO KWA KUOA MKE KUZIDI UMRI WAKE?
Tags:
Shirikisha
-
▶ Jibu Hoja Hii