FotoBaraza.Net

Don Magere

CHA!!!Kiswahili chetu cha kuandika ni kibaya na kibovu!!!!!!

CHA kipindi cha nyuma ulikuwa makini katika kukosoa wale wote wenye matumizi mabovu ya kiswahili lakini kwa sasa umeacha kazi hiyo. Kiswahili kibovu kimeibuka kwa kasi ya ajabu kama wamachinga walivyorudi katika mitaa ya Kariakoo na kule kati posta.
CHA chukua RUNGU lako ulilokabidhiwa na kijiji ili uwashikishe adabu hawa wachafuzi wa Lugha.(hapa simaanishi kiswahili cha kihuni)
Ni kiswahili hiki cha kawaida ambacho kwa mfano badala ya mtu kuandika
ADHA anaandika HADHA
HIZI anaandika IZI
AIBU anaandika HAIBU
DHARAU anaandika ZARAHU
Kuna mengi zadi ila nimetaja machache tu
Inakera sana na inakatisha tamaa kusoma maoni ya mtu kama makosa ya namna hiyo yanajirudiarudia.
Chonde chonde CHA take action please!

Shirikisha Twitter

Jibu Hoja Hii

Michango ya Mjadala Huu

nakuunga mkono; natumaini Cha mwenyewe yuko poa kabisa tunapokuja katika suala hili...kazi njema Cha!

Jibu Hoja Hii

Ok. Dada Sophie, nitaanza kutekeleza

Jibu Hoja Hii

Hata mimi lugha ya namna hiyo huwa inanikera hasa kila nisomapo ujumbe wenye makosa ya kisarufi kama haya ambayo yanaweza yakarekebishika!

Jibu Hoja Hii

Pascal, naomba uoneshe kila kazi ya kiambishi katika neno YAKAREKEBISHIKA, maana inaonesha upo makini katika KISWAHILI

PamoJah

Jibu Hoja Hii

Lugha/maandishi matamu humvutia msomaji, haswaa sisi tuliosoma muandiko na sarufi! Kiukweli wengi wetu hudharau sana kile tuandikacho, na hiyo inaonesha kuwa huwa tunaandika bila kurejea maandishi yetu kabla ya kuyaweka kwa ajili ya kusomwa na wadau wengine. Tujitahidi kuandika vizuri ili kutupa ladha ya kile kiandikwacho!

Jibu Hoja Hii

Umesema kweli Mkuu Stiba. Unajua kuna mambo mengi tu huwa nawasikia hata wale waitwao waheshimiwa pale bungeni. Kwa mfano utamsikia mbunge akisema "kwa niaba yangu" na "kwa niaba ya fulani", kweli hivi hiki ndicho Kiswahili tulichofundiswa darasani na walimu wetu kweli? Au haya ni matokeo ya kufundishwa na walimu ambao walifeli?

Jibu Hoja Hii

Tatizo letu watanzania huwa tunajifanya tunaongea "slang" ya kiswahili, wakati hata kiswahili chenyewe fasaha hatukijui! Kwa mfano ukitaka kusikiliza kiswahili fasaha uwe mtazamaji wa kipindi cha lugha yetu cha TBC1 uwasikilize kina Mochiwa na wenzie wanavyoongea kiswahili mpaka utasikia raha!

Jibu Hoja Hii

Tatizo bado tunataka kuongea Kiswahili kwa kufananisha na lugha ya Kiingereza (English). Wewe wasikilize watangazaji mbalimbali hasa wa hizi radio binafsi wanavyoharibu Kiswahili, na hawa ni chanzo cha kupotosha kiswahili, wengine ni wabunge yaani mimi huwa nacheka sana mkuu Stiba, hata humu ndani wamo wengi sana, sasa kwa mfano maneno kama hayo yaliyoorodheshwa na Lecturer Magere kweli yanatia hasira sana, eti mtu na kwa nguvu zote na kwa kujiamini anasema HAIBU badala ya AIBU, ZARAU badala ya DHARAU na mengine mengi tu.

Jibu Hoja Hii

Dawa yao ni kumpa Lecture Magere kazi ya "Kifimbo cheza", kila atakaeharibu lugha ama kwa kuandika au kwa kuongea atachezea bakora mpaka anyooshe! Au unaniambiaje mkuu CHA?1

Jibu Hoja Hii

Stiba. The great CHA anaiweza sana kazi hii hivyo tumwachie nafasi aifanye kazi yake.Ila kama ataomba msaada basi hapo hatunabudi kumsaidia!

Jibu Hoja Hii

Ni kweli Dr Stiba mwandiko wako ni mzuri, maana ni kama vile unapigisha chapa. Nakumbuka notice zako zilivyokuwa zikisambaa, kila mtu akipenda kusoma maandishi yako na ya God Sula.

Jibu Hoja Hii

Hahahahahaaaa, Pascal we acha tu, mwandiko huo ulinisababishia kupoteza madaftari mengi sana ya notes hasa yale aliyokuwa akiazima Big Emma!

Jibu Hoja Hii

RSS

Besdei za Kuzaliwa

© 2010   Created by Babukadja on Ning.   Create a Ning Network!

Beji  |  Report an Issue  |  Faragha  |  Terms of Service

Sign in to chat!
Free Web Counter
Hit Counter