FotoBaraza.Net

CHA the Great

ALFANI APATA ZAWADI YAKE KATIKA SHINDANO LA *SHINDA MUDA WA MAONGEZI WA 50000/- (ELFU HAMSINI) AU LUNCH HOTEL YA KILIMANJARO 'MARUDIO' ZAWADI IMEONGEZWA*.

Kwanza kabisa naomba radhi kwa usumbufu uliotokea kwa Bw. Dismas na wanakijiji kwa ujumla kutokana na hitilafu ya lugha. Kutokana na malalamiko ya wadau tumekubaliana kuwa shindano hilo lirudiwe. Na mdhamini wa shindano hili ameahidi kuongeza zawadi ya muda wa maongezi kutoka 30000/- hadi 50000/- za Kitanzania. Katika shindano hili majina yafuatayo hayatoruhusiwa kushiriki katika shindano hili kwa kujibu maswali. Majina hayo ni Michuzi Jr. ambaye ni Balozi, Oswald Akyoo ambaye ni Mdhamini, Dismas, Cha, ambaye ni muanzilishi wa PamoJah na Mkuu au Mwenyekiti wa kijiji hiki Babukadja.

Maelezo mafupi juu ya maswali. Andika herufi unayoona ni sahihi katika kila swali au andika SI KWELI kwa swali unarofikiri halina usahihi na KWELI katika swali unalofikiri ni sahihi na kujaza sehemu iliyowazi au kutaja kinachotakiwa kutajwa.

1.Mwanachama yupi alitoa wazo la kuchapishwa t-shirts za PamoJah? A. Babukadja B. Dismas C. Michuzi Jr.
2. Taja majina mawili ya wana PamoJah waliopewa onyo kutokana na utovu wa nidhamu hapa kijijini.
3. Taja majina 15 ya wanachama wa PamoJah waliojiunga Baada ya Tarehe 23-Dec-2009.
4. A. Magere B. Mujydbubz C. Lucie wa Mama, D. Vadonde, E. George Rutenge mmoja wao ni wa kwanza kuvaa t-shirt ya PamoJah.
5. Chaoga, Mtoto Mzuri, Pascal, Ndekia, Michuzi Jr. Dismas ni wanachama wa PamoJah kwa sasa.
6. Taja jina la Muanzilishi wa FOTOBARAZA FONDATION.
7. Taja jina halisi la Mkuu wa Malavidavi ( Love Affairs)
8. Young alitembelewa na wana PamoJah 5 waliokwenda kumpa pole kutokana na msiba wa mama yake (YOUNG), taja majina yao.
9. Taja jina la msanii wa kiume aliyewahi kuonekana katika mchezo wa kuigiza akiwa amevaa T-shirt ya PamoJah katika kituo cha ITV.
10. Taja jina la msanii wa kike aliyewahi kuonekana amevaa t-shirt ya PamoJah katika mchezo wa kuigiza katika kituo cha ITV.

SHINDANO HILI LITAISHA SIKU YA ALHAMISI TAREHE 17-9-2009, SAA SITA MCHANA
KUJIBU MASWALI NI MARA MOJA TU, MSHIRIKI ATAKAYESHIRIKI ZAIDI YA MARA MOJA ATAKUWA AMEJITOA KATIKA SHINDANO HILI. ZAWADI KUTOLEWA NA MDHAMINI WA SHINDANO HILI, BWANA OSWALD JOHN AKYOO.
ZAWADI HAITABADIRISHWA KWA FEDHA.

PamoJah
na senksi so mach indidi!!!

Shirikisha Twitter

Jibu Hoja Hii

Michango ya Mjadala Huu

Ha ha ha Teh teh! Mkuu CHA nilitegemea ungeijibu hoja yangu kwanza kisha tuone kama kweli Dismas ni mshindi au kuna mwingine aliyestahili kushinda!
Nadhani kwa walioshiriki kujibu lile shindano la kwanza hawakupata shida wala kuchanganyikiwa na lugha iliyotumika.hivyo walijibu kwa kwa kadri ya walivyooelewa.
Mimi nadhani wewe mwandaaji ndo lugha imekugeuka maana hukutegemea kama watu tungeelewa jinsi tulivyoelewa,haswa kipengele cha nani mwanachama kwa kwanza kujiunga na Pamojah!

Kwahiyo kwa mtazamo wangu kulikuwa hakuna haja ya kurudia shindano isipokuwa tungeangalia ninani kajibu vizuri kutokana na mazingira ya lugha iliyotumika na huyo ndo angekuwa mshindi.

N.B naaomba ufafanue umetumia vigezo gani kubatilisha matokeo na kuamua kurudia shindano!!!!!!

Jibu Hoja Hii

Mkuu wangu Lecturer wangu, nimekuwa nikiomba maoni kwa wadau wa kjiji kuhusiana na shindano lile, karibia wote wamependekeza shindano lirudiwe. Ni hayo tu Lecturer wangu.

Asante sana.

Jibu Hoja Hii

rekebisha swali la tatu CHA the great. au nijibu hilo swali kwamba mpaka sasa hakuna wanachama 15 waliojiunga na PamoJah baada ya tarehe 23 Dec 2009

Jibu Hoja Hii

Mkuu Pascal unawapoteza wenzako sawa tu.

Jibu Hoja Hii

Mpaka sasa CHA the Great hujabadilisha swali la tatu?

3. Taja majina 15 ya wanachama wa PamoJah waliojiunga Baada ya Tarehe 23-Dec-2009.
hakika hatujaifikia tarehe 23 - Dec - 2009. kwahiyo hamna wanachama 15 waliojiunga na PamoJah baada ya hiyo tarehe mpaka sasa. Labda tusubiri mwakani.

Jibu Hoja Hii

Mbona haya maswali haya husiki na mfumo wa kujibu kweli au si kweli? hebu tutafunie kidogo hapo sali gani na gani ndo ya kujibia huo mfumo? duh!

Jibu Hoja Hii

Loo nijibu tena nishinde kisha mizingue ianze hapa kila mtu mzima ila mambo yanayotendeka hayaelekei...sikutegemea kama cha utachukua uamuzi huu ambao unadhihirisha udhaifu wako...ulipaswa uombe kwanza msamaha wanakijiji kisha ukasikiliza maoni yao...ila sikukurupuka...GUD day

Jibu Hoja Hii

And nafikiri CHA unahitaji msaada kuandaa maswali me naona umekurupuka mradi ipite..soma vizuri maswali utanielewa...

Jibu Hoja Hii

Na ushauri wa bure CHA uongozi ni kazi unaweza ukamiliki kitu fulani ila kukiongoza ukashindwa...jibu hoja za watu,ulipokosea omba msamaha kisha sikiliza maoni yao watasemaje...

Jibu Hoja Hii

Nawatakia AMANI na UTULIVU ktk shindano hili. 2po pa1

Jibu Hoja Hii

Kazi ipo! naona wadau wamekasirishwa sana na uhamuzi wa kulirudia pambano! mimi sioni sababu ya kuitilafiana kwa mambo madogo kama haya! ......Naomba busara zitumike kulitatua tatizo hili!

Jibu Hoja Hii

Naona hilo ni swali la mtego tu, usifungue watu macho

Jibu Hoja Hii

RSS

Besdei za Kuzaliwa

© 2010   Created by Babukadja on Ning.   Create a Ning Network!

Beji  |  Report an Issue  |  Faragha  |  Terms of Service

Sign in to chat!
Free Web Counter
Hit Counter